Kurunzi Wanawake leo inamuangazia Aziza Nassib, mjasiriamali kutoka Dodoma Tanzania ambaye licha ya hofu ya kuonekana kichaa, ameamua kuokota makopo na chupa za plastiki ambazo anazichakata na kuzifanya mali ghafi. Unapoishi mjini, lazima uisumbue akili ili ujipatie kipato cha halali, ndivyo anavyofanya bi Aziza.